The House of Favourite Newspapers

Hii sasa kali! Idriss, Madee wapeana za chembe

0

MSHINDI wa Big Brother Africa mwaka 2014, Idriss Sultan na msanii wa Bongo Fleva Madee Ally a.k.a ‘Shineida’ wamerushiana madongo kwenye mtandao ya kijamii wa Twitter.
Idriss alianza kuuwasha moto kwa kuandika maneno yafuatayo kwenye ukurasa wake wa Twitter:
“Ukiona msanii ana nyimbo mbaya jua moja tu, ana marafiki wanafiki balaa, yaani ni waongo ile mbaya.”

Baada ya kuiona posti hiyo, ndipo Madee akavunja ukimya kwa kukomenti maneno ambayo mashabiki wameyatafsiri kama dongo kwa Idriss.
“Na je ukiona kijana kapata hela nyingi na zikaisha ghafla na yeye ana marafiki wa aina gani?”

NA ISRI MOHAMED/GPL

Leave A Reply