The House of Favourite Newspapers

Kim Nana Haachiki Kirahisi

Image result for kim nana tanzania

WALE mnaopenda kufuatilia maisha ya watu mpo? Haya sasa muuza nyago maarufu Bongo Lilian Kessy ‘Kim Nana’ amesema kuwa yeye kuachika siyo rahisi kama watu wanavyodhani au wanavyoomba iwe kila siku anajiamini ni msichana mzuri.

 

Kim Nana aliiambia Mikito Nusunusu kuwa mikwaruzano katika uhusiano lazima itokee hivyo hata yeye ametofautiana kidogo tu na mpenzi wake Tonny Albert ’T Bway’ lakini siyo kama wameachana kama ambavyo watu wanazusha na kibaya zaidi ni kwamba asilimia kubwa ya watu wanapenda kusema mambo ambayo hawana uhakika nayo.

Image result for kim nana na Tbway

“Jamani eti nimeachika na kipigo juu, mimi siwezi kuachika kirahisi hivyo kama wanavyofikiria najiamini sana, sasa watu wanapenda kuongeaongea tu mambo wasiyokuwa na uhakika nayo.“Kutofautiana katika uhusiano ni jambo la kawaida sana tu, kwa sababu hata hao wanaoongea kuhusu mimi huwa wanagombana na watu wao wakaribu,” alisema.Nana haachiki kirahisi.

Comments are closed.