WAZIRI Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa sambamba na Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema jana wameungana na viongozi wengine wa chama kumnadi mgombea wa chama hicho Yonas Laizer katika kata ya Meserani, eneo la duka bovu.
Lowassa akimnadi mgombea huyo amesema hatishwi na idadi ya wabunge wa ccm waliyopangwa kuja kupambana naye katika uchaguzi huo. Amesema hata wakija zaidi ya mia moja Kalanga hatopata ushindi.
“Numesikia wamepanga wabunge 16 kuja kupambana na sisi.Nasema hata waje zaidi ya mia moja tutawanyoosha,” alisema Lowassa huku akishangiliwa.
Comments are closed.