The House of Favourite Newspapers

Madee, Lulu Mahaba Niue!

1
Madee Lulu Diva kwenye penzi zito.

 

STAA wa Bongo Fleva anayejiita Rais wa Manzese, Hamad Ally ‘Madee’ na staa mwenzake wa muziki huo, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ wameibua minong’ono baada ya kuonekana wakiwa wamegandana kama ruba huku wakioneshana mahaba niue.

 

Mastaa hao walibambwa juzikati wakiwa ‘ziro distansi’ kwenye shoo ya miaka 15 ya staa wa Nyimbo za asili, Saida Karoli ndani ya Ukumbi wa Escape-One uliopo Mikocheni jijini Dar.

 

 

…Waki-enjoy

 

Madee ni miongoni mwa mastaa wakongwe ambao hawajaoa wala kutambulisha wachumba, zaidi ya kumtambulisha mwanaye wa kike aitwaye Saida bila kumuweka wazi mama yake.

 

Katika event hiyo ambayo Wikienda lilikuwa ni miongoni mwa vyombo vya habari vilivyokuwa vikifuatilia na kuchukua matukio mbalimbali, lilibahatika kumuona Madee na Lulu Diva wakiingia mapema kabisa ukumbini hapo huku wakiwa wamegandana kwa staili ya mume na mke.

 

 

Wakiondoka eneo hilo.

 

 

Hali hiyo iliendelea kujidhihirisha muda wote wa shoo hiyo ambapo wawili hao walikaa sehemu moja huku mazungumzo yao yakiwa ya kimahaba na kuitana majinamatamumatamu kama ‘baby’ na kukumbatiana kila wakati.

 

Baadhi ya mashabiki wao walihisi labda kwa sasa ni wapenzi rasmi kwani hawakuwa wakijifi cha ambapo ilifi kia hatua hata msalani wakawa wanasindikizana.

 

Haoo, wanasepa zao

 

Tofauti na mastaa wengine, wawili hao hawakuogopa hata kamera za mapaparazi waliowafuata na kuwafotoa picha mahali walipokuwa wameketi, jambo ambalo lilikuwa likiwaaminisha wengi kuwa ni wapenzi wa muda mrefu kwani hata muda wa kuondoka walionekana wakitembea wakiwa wameshikana mikono na interview mbalimbali walifanya pamoja.

 

STORI: MUSA MATEJA | IJUMAA WIKIENDA| DAR

Mshuhudie LIVE Mtanzania Mrefu Kuliko Wote na Mateso Anayoyapata

1 Comment
  1. […] Madee, Lulu Mahaba Niue! […]

Leave A Reply