Mastaa na Heshima kwa Mwanamke
TANGU mwaka huu uanze, mstaa mbalimb ali wameonesha dhamira ya heshima ya mwanamke katika jamii katika suala zima la kuwa mama.
Listi ya mastaa waliojifungua mwaka jana haikuwa kubwa kivile kuliko mwaka huu kwani waliofanikiwa kujifungua mwaka jana ni Zari na Chuchu Hans.
Lakini kwa mwaka huu pekee ndani ya miezi miwili mitatu mastaa kibao wameshajifungua na wengine wakiwa mbioni kujifungua. Miongoni mwa mastaa hao ni pamoja na Linah, Coletha Raymond, Meninah, Millen Magese, Esha Buheti na Hamisa Mobeto.
HAMISA MOBETO
Ni mwanamitindo mwenye jina kubwa Bongo na mwenye kujituma katika kazi yake. Baada ya kuwa na mtoto mmoja wa kike, hivi karibuni ameongeza mwingine wa kiume.
FAIZA ALLY
Kama ilivyokuwa kwa Mobeto, Faiza naye anasimama kama mwanamke mwenye kujituma katika sanaa ya filamu. Ameongeza mtoto wa kiume hivi karibuni baada ya kuwa na mmoja wa kike.
MILLEN MAGESE!
Ni mwanamitindo wa kimataifa aliyesota kwa miaka zaidi ya kumi katika kutafuta mtoto. Hivi karibuni aliwashangaza wengi baada ya kufanikiwa kujifungua mtoto wa kiume.
LINAH!
Ilikuwa kama utani kwa msanii huyu wa Bongo Fleva kuamua kubeba ujauzito kutokana na wengi kujikita zaidi kwenye muziki. Kwa sasa ameshajifungua mtoto wa kiume.
ESHA BUHETI!
Juzikati ilifanyika ‘baby shower’ ya kumkaribisha mtoto wake wa pili ambaye kwa mujibu wa vipimo ni wa kike hivyo akijifungua atakuwa na watoto wa kike wawili.
NA MWANDISHI WETU, IJUMAA
====