MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Kazi, imeamuru mitambo ya kufua umeme ya Kampuni ya Symbion Power kupigwa mnada baada ya kushindwa kuwalipa mishahara wafanyakazi kwa miaka mitatu.
Katika utekelezaji wa amri iliyotolewa, tangazo limewekwa katika ofisi za kampuni hiyo. Baadhi ya wafanyakazi wamesema wanadai zaidi ya Sh. bilioni 12 na wanaotakiwa kulipwa ni 43.
Wafanyakazi wanadai mishahara ya miezi zaidi ya 30 na wamekuwa wakifanya kazi kwa kipindi chote wakiamini watalipwa #Haki zao.