Video: Polisi Watoa Ufafanuzi Kuhusu Kukamatwa Kwa Geofrey Mwambe

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewahakikishia wakazi wa jiji hilo kuwa hali ya usalama inaendelea kuwa nzuri na kwamba wananchi wanaendelea na shughuli zao za kila siku bila wasiwasi.
Kupitia taarifa iliyotolewa leo Desemba 12, 2025 na ofisi ya Kamanda wa Kanda Maalum ya Polisi, imeelezwa kuwa pamoja na utulivu huo, mnamo tarehe 07 Desemba, 2025, majira ya usiku katika eneo la Tegeta Kinondoni, polisi walimkamata Geofrey Mwambe kwa tuhuma za kuhusika na makosa ya jinai ambayo bado yanafanyiwa uchunguzi.
Jeshi la Polisi limesema hatua zaidi za kisheria ziko mbioni kukamilishwa mara baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.


