The House of Favourite Newspapers

Raha ya chakula mboga

WANAKWA-MBIA jogoo anawika lakini hawezi kutaga! Heri yangu niliyevaa mtandio kuliko weeweee unayeanika makalio heee heeeiyaaaa! Na utachuna mwaka huu, ukiona mikono haitakati kwa kunawa basi chukua nguo ufue, hebu tupishe siye tuliokulia mjini tutulie bibi weeee!  Kama nakuona jicho kodo kutaka kujua mada yangu ya leo inamaanisha nini! Mboooona! Shoga mji mzito huuu! Yaani dunia imejaa lawama kuliko shukurani, sawa hatukatai masikio huonja maneno kama kama ulimi unavyoonja chakula! Waswahili wanasema siyo lazima upate samaki hata kupanda mtumbwi na mvuvi tu kuna faida yake, upo nyonyo?

Nimejaa tele Anti Naa Shangingi lililokwepa mishale mingi! Ukisikia kubwa la maadui ndiyo mimi, mikono spana, miguu jeki! Zubaa tu kutwa kubadilisha madela uone kama hatujaolewa tunaojua kulikunja lemba! Wareeee reeeee! Hebu tuingie kwenye kileee ambacho kimenikutanisha mimi na wewe leo hii maana kuna watu sijui niwafunde vipi lakini bado wanakuwa hawaelewi! Tuelezane ukweli hivi chakula bila mboga kinanoga kweli?

Leo sikung’ati sikio bali nakupasha upashike mwanamke wewee! Sitaki kuzungumzia kabila hata moja lakini inatakiwa tubadilike! Mwanamke mzima unakuwa mgomba usiotoa ndizi basi bora ukatwe tujue moja kama tutawapa ng’ombe au tutandike chini tuchinjie mbuzi.

Tena uelewe shoga yangu hapa nilipo mwenzenu limenifika hapa! Malalamiko kila siku nayapokea hadi imekuwa kero sasa lakini inabidi tu nifungue kundi la WhatsApp ili tupashane mkapashika, tufundane huko mkafundika na hii ni kwa wanawake wenzangu tu!

Kama unavyojua shoga, koo langu likinikauka huwa napenda kutafuta sehemu iliyotulia nashusha zangu moja au mbili baridi narudi nyumbani! Basi siku hiyo nimekaa zangu si akanifuata mwanamke mwenzangu mmoja na kunisogelea akidai ananijua! Mwanzoni niliona kama ni tapeli wa mjini kumbe anakisebusebu kinachomsumbua!

Akaniamkia na kuanza kuomba ushauri bila kujua amekutana na kungwi wa makungwi! Anasema imekuwa kawaida kwa mumewe kumuonesha kuwa hamhitaji faragha na kuna wakati anamtamkia maneno ya kuudhi kuwa kwa sababu ya kuwa mgomba ndiyo maana amemuacha.

Nikamuuliza; kulikoni shoga ukawa mgomba! Si ndiyo akaendelea kutapika kuwa hakuwahi kufundwa, kiuno chake kigumu kama mkokoteni wa kijiji! Looo ngachoka! Nikugeukie sasa na wewe mwanamke mwenzangu unayenisikiliza! Jamani chakula bila mboga kikanoga? Mwanamke lazima ujue kumuandaa mwanaume wako kwenye sita kwa sita hii itamfanya na yeye awe mwepesi kumalizia maandalizi.

Siyo umejiweka bubu kama sanamu la Samora lililoshika mtutu, hata kutoa vigelegele hujui unachojua kuuliza umemaliza! Shuuuutuuuu! Shoga mwanamke ujue kuzitumia kucha, ujue kuutumia ulimi na mwisho ujue kukata feni.

Kwa leo nisiwe muongeaji sana, kama nilivyowaambia kwa wasomaji wangu tu mnaweza kuwepo kwenye makundi yangu manne ya WhatsApp yanayoitwa Shangingi Mstaafu na unaweza kunitumia meseji au kupiga kwa maelezo kupitia namba zangu; 0713 76 11 35. Ni mimi Shangingi Mstaafu Anti Nasra ukipenda niite Anti Naa!

Comments are closed.