KIKOSI cha Simba leo kimefanya mazoezi kwenye uwanja wa Boko Veterani uliopo Ununio jijini Dar ikiwa ni maandalizi ya bonanza lake la Simba Day linalotarajiwa kufanyika kesho Uwanja wa Taifa.
Katika mazoezi hayo kikosi hicho kiliwajumuisha wachezaji wake wapya akiwemo Haruna Niyonzima, John Boko, Emmanuel Okwi, Aishi Manula, Said Mohammed, Erasto Nyoni na wengineo.
Baada ya mazoezi
Baada ya mazoezi hayo mashabiki waliofika kuangalia jinsi simba ilivyopasha walishindwa kuzuia hisia zao na kuamua kulisukuma gari la Niyonzima huku wakimshangilia na kumkaribisha.