The House of Favourite Newspapers

Ujio Mpya wa Bad Boy Tanzania Isimame Kidogo!

0
Ujio Mpya wa Bad Boy
Ibrahimu Mbwana ‘Bad Boy’.

 

MSANII  wa filamu Tanzania, Ibrahimu Mbwana ‘Bad Boy’, aliyewahi kutamba kwenye filamu kama Misukosuko , Double J na nyingine nyingi, amerudi kwa kishindo na filamu yake inayoitwa Radhi Ya Mama.

 

“Nimekaa kimya kwa muda mrefu, na hii ni kutokana na kwamba nilikuwa nafanya uchunguzi kwanza soko la filamu linahitaji nini, baada ya kupata majibu, ndiyo nikaingia lokesheni kutengeneza filamu yangu ya Radhi ya Mama ambayo nitaizindua rasmi Jumapili ya Agosti 20, mwaka huu katika ukumbi wa MRC uliopo Mikocheni.

 

“Naomba watu wafike siku hiyo washuhudie ujio mpya wa Bad Boy, kiingilio itakuwa ni shilingi elfu 10,  ambapo kila mtu atapata chakula na kinywaji bure, pia kutakuwa na burudani mbalimbali kutoka kwa wanamuziki wa Hip Hop, Singeli, ngoma za asili na maonyesho ya mitindo,” amesema Bad Boy.

Ujio Mpya wa Bad Boy

Bad Boy alikuwa bondia kabla ya kuzamia kwenye uigizaji, ambapo alinga’ra zaidi kwenye muvi alizoshirikiana na muigizaji mwenziye  J Plus.

 

Usiache kuicheki interview ya Bad Boy katika Global TV Online.

 

NA ISRI MOHAMED/GPL

Leave A Reply