UKATILI WALIOFANYIWA WATUMWA KUTOKA AFRIKA HUKO AMERIKA
PICHA za kusikitisha zilizopigwa miaka zaidi ya 150 iliyopita zinaonyesha ukatili wa kutisha waliokuwa wanafanyiwa watumwa kutoka Afrika waliosombwa kupelekwa barani Amerika kwenda kufanyishwa kazi ngumu.
Huko walichapwa mijeledi, wakafanyishwa kazi nzito kama wanyama kwenye mashamba ya pamba na miradi ingine migumu wakitishwa kwamba polisi wangewasaka popote na kuwakamata iwapo wangethubutu kutoroka.
Picha hizo zimeibuliwa katika kumbukumbu ya kutimia mwaka wa 153 tangu kupigwa marufuku kwa utumwa nchini Marekani, Januari 1, 1865 kufuatia Badiliko la 13 la Katiba ya nchi hiyo ambalo lilisainiwa na Rais Abraham Lincoln, Februari 1, 1865.
Miongoni mwa picha hizo ni pamoja na zilizopigwa mnamo miaka ya 1700 zikionyesha maisha ya watumwa nchini Marekani ambapo kuna moja inayoonyesha mgongo wa mtumwa ulivyochanwa kwa mijeledi na picha nyingine nyingi zikionyesha wakifanya kazi za kitumwa kwenye mashamba ya pamba.
WALUSANGA NDAKI/MITANDAO/MASHIRIKA YA HABARI
Comments are closed.