The House of Favourite Newspapers

Vyakula Vya Kula Kwa Mgonjwa Wa Vidonda Vya Tumbo

0

LEO tutaangazia vyakula vya kuepukwa na wagonjwa wa vidonda vya tumbo lakini pia tutaeleza vyakula vinavyofaa kuliwa na hao wenye matatizo hayo. Ili kupunguza makali au kujiepusha kabisa na ugonjwa huo wa vidonda vya tumbo (ulcers), unapaswa kujiepusha kula vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi.

 

VYAKULA VYA KUEPUKWA

Kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo anatakiwa aepuke kula vyakula aina zote vilivyopikwa na kuungwa viungo vingi vya aina mbalimbali (mchanganyiko) kama sambusa za pilipili, achali (pickle), juisi ya ukwaju, juisi ya limau n.k. Viungo vingine visivyofaa kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo ni pilipili kali za aina zote na viungo vingine vyenye ladha ya ukali au uchachu ambavyo hutiwa ndani ya mboga au chakula ili kuongeza ladha kama vile vinegar au tangawizi.

Pombe na kahawa au vinywaji vingine vyenye caffeine, vinaweza kuleta matatizo kwa mtu mwenye vidonda vya tumbo na kwa mtu asiye navyo anaweza pia kupatwa na tatizo hilo. Hivyo basi ni vyema wagonjwa wa vidonda vya tumbo au hata kama huugui, inashauriwa kuepuka vyakula hivyo na kama unavitumia basi tumia kwa kiasi kidogo kwani kwa mfano vinywaji vyenye caffeine huongeza asidi tumboni na hivyo vinaweza kusababisha vidonda au kuzidisha maumivu kwa anayeumwa.

UHUSIANO KATI YA ULAJI CHUMVI NA VIDONDA VYA TUMBO

Mgonjwa anashauriwa kuepuka ulaji wa vyakula vyenye chumvi nyingi, hususan vyakula vya kusindika ambavyo huwekwa

JINSI ULIVYO INATOKANA NA UNAVYOKULA

Vyakula vya kuepukwa na mgonjwa wa vidonda vya tumbo chumvi nyingi ili visiharibike haraka. Pia jiepushe na kuongeza chumvi kwenye chakula wakati wa kula, yaani chumvi mbichi inayotiwa mezani wakati wa kula si nzuri kiafya.

Wagonjwa wa vidonda vya tumbo wanashauriwa kula mafuta yatokanayo na samaki ambayo kitaalamu huitwa Omega-3 Fats ambayo yameonekana kutoa ahueni kwa wagonjwa. Kwa mtu ambaye si mgonjwa wa vidonda vya tumbo akila mafuta hayo atakuwa anajiwekea kinga dhidi ya vidonda vya tumbo na magonjwa mengine ya tumbo.

Ulaji wa vyakula vyenye madini na vitamini kwa wingi husaidia pia kuleta ahueni kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo na kutoa kinga kwa wale ambao hawajaathirika. Wenye vidonda vya tumbo wanashauriwa kupenda kula matunda na mboga za majani kama vile karoti, juisi ya kabeji, ndizi mbivu na matunda mengine yenye vitamini C, hali kadhalika maziwa ya mbuzi, jibini na cream za maziwa, kwani huleta ahueni kwa wagonjwa hao.

Sigara ni mbaya kwani huongeza hatari ya mtu kupatwa na ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na wasiwasi. Kuepukana na maradhi hayo, watu wazingatie ulaji sahihi ili waweze kuishi maisha ya furaha.

Usipitwe na Matukio, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers

Android ===>Google Play

iOS ===>Apple Store

Leave A Reply