The House of Favourite Newspapers

ZARI AFUNGUKIA MWILI WAKE

Zarina Hassan ‘Zari The bosslady’

MWANAMAMA ambaye ni mzazi mwenziye na staa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, Zarina Hassan ‘Zari The bosslady’ ame­wafunda wanawake jinsi ya kutengeneza mwili kama ulivyo wake. 

 

Akizun­gumza na Za Motomoto alipokuwa akitoa msaada ka­tika Hospitali ya Mbagala jijini Dar al­isema kuwa, mwili wake kuonekana vile ingawaje ameshazaa ni kwa sababu anakula vyakula vya afya.

 

“Unajua hakuna kitu kizuri sana kwa mwa­namke tena aliyezaa kula vyakula visivyo na wanga kwa wingi na kupunguza mafuta kwa sababu ndio vinavyofanya mwili kuongezeka badala yake wale vyakula vya Vitamini zaidi kama mboga za majani, matunda itawasawaidia sana hii ndio siri yangu kubwa watoto watano lakini naonekana vizuri,” alisema Zari.

Stori:Imelda Mtema, Dar

Comments are closed.