Mwanaume hata awe bahili vipi, hawezi kumpa mwanamke mimba nusu.
Kama ubinadamu kazi mbona hatupewi mishahara?
Ukichanganya wali na choroko unapata mseto, lakini hautibu malaria.
Hata Moshi ni mji lakini hautokani na moto
Hata uwe na haraka vipi kwenda Zenji, huwezi kupanda Jahazi ya Mzee Yusuf
Umeme hauna kiuno lakini unaongoza kwa kukatika
Hata kizibo ni mfuniko lakini hauwezi kufunika sufuria
Hata uwe na heshima vipi huwezi kumpokea askari bunduki..
News are shaking can you stop it please