Na Hamida Hassan
Staa wa filamu ya ‘Best Man’, Mariam Ismail ameibuka na kusema kuwa utulivu wake ndiyo unamfanya awe na staha ya usanii mpaka leo na angalizo kwa mapeshee ni kwamba, yeye siyo maharage ya Mbeya (siyo rahisi kuingilika).
Akizungumza na Ijumaa juzikati, Mariam alisema kuwa mpaka sasa ameweza kujikinga na wanaume wakware kwa kuwa amejiwekea utaratibu wa kuwa mbali na wasumbufu wa mapenzi kwa kutumia pesa zao.
“Unajua ukiamua kuweka heshima yako unaweza pamoja na ustaa kwani kuwa staa siyo sababu ya kutoka na kila anayekutamani eti kisa ana pesa,” alisema Mariam.