×

Macho ng’aring’ari kwa kutumia juisi ya nanasi!

Jinsi ya kutumia juisi hiyo
Chukua nanasi kipande, kikamue maji yake kidogo kisha paka chini ya macho.
Baada ya hapo acha kwa muda wa dakika 20 kisha osha, ifanye iwe tabia yako kila siku kwa ajili ya kuondoa mikunjo ya ngozi.
Tiba hii itaifanya ngozi yako kuteleza, kuwa laini na kuiweka mbali na mikunjo inayosababisha uwe na muonekano wa kizee.

Pia papai na asali
Papai pia ni tunda ambalo lina uwezo wa kuondoa mikunjo kwenye macho na kukufanya usahau uzee.

Unafanyaje?
Chukua papai, limenye kisha lichote kwa kijiko na uchanganye na asali kijiko kimoja. Baada ya hapo paka mchanganyiko huo chini ya macho yako, kama unapenda unaweza kupaka uso mzima. Hii itasaidia kuirudisha ngozi yako iliyokufa na kukufanya uwe  ng’aring’ari.

Leave a Comment