×

Baraka, Najma wagandana kama ruba

11374089_541731639330311_1460164552_nBaraka Andrew ‘Barakah Da Prince’ na Najma Dattan ‘Naj’

Mkali wa Ngoma ya Siwezi, Baraka Andrew ‘Barakah Da Prince’ amejikuta akilazimisha ile kauli ya abiria chunga mzigo wako, kutokana na kutompa mwandani wake, Najma Dattan ‘Naj’ nafasi ya kujiachia na watu wengine klabu na kugandana kama ruba.

Tukio hilo lilijiri wikiendi iliyopita kwenye Ukumbi wa Maisha Basement uliopo Kijitonyama jijini Dar kulipokuwa na shoo ya Usiku wa Pam D na Young D ndipo wasanii hao walitinga usiku mnene wakionekana kuwa beneti muda wote, hata pale mmoja wapo aliposalimiana na watu wengine hakumuachia mkono mwenzake kuhofia wajanja wangemshobokea.

Kutokana na ishu hiyo ambayo iliwafanya watu wabaki wakiwakodolea macho mwanzo mwisho, walipoulizwa waliishia kucheka na kudai kinachosababisha hali hiyo ni mahaba mazito waliyonayo.

KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, DOWNLOAD NA INSTALL APP HII ILIYOPO KWENYE PLAY STORE YAKO==>VODACOM M-PAPER APP

*********

JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:

KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA

INSTAGRAM: @Globalpublishers

TWITTER: @GlobalHabari

FACEBOOK: @GlobalPublishers

SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers

GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com

HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz

Leave a Comment