×

Sheikh Mkuu Akerwa Tabia za Akina Wema

Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa Salim

Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa Salim.

Stori: Gladness Mallya, Risasi Jumamosi

DAR ES SALAAM:  Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa Salim amesema anakerwa na mastaa wanaodaiwa kuwa na tabia chafu zenye viashiria vya usagaji.

Shehe huyo aliyasema hayo hivi karibuni baada ya kutafutwa na gazeti hili kufuatia kusambaa kwa picha mitandaoni zinazomuonesha mwigizaji Wema Sepetu ‘Madam’ akiwa kwenye pozi la kimahaba na mwanamuziki Diana Exavery ‘Malaika’.

wema

Wema Sepetu

“Vitendo hivyo vinavyoashiria tabia za usagaji ni machukizo kwa Mwenyezi Mungu, pia ni laana na havikubaliki kabisa katika imani yeyote, anayefanya vitendo hivyo anatakiwa kuachana navyo maana havimpendezi Mungu.

“Wasanii wote, wanapaswa kutambua kuwa wao ni kioo cha jamii na watu wanahitaji kujifunza mambo mengi mazuri kutoka kwao na si kuwapotosha,” alisema Shehe Alhadi.

wema-aunt

Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wakiwa katika pozi tata.

Ikumbukwe kuwa hii si mara ya kwanza kwa Wema Sepetu kujianika akiwa kwenye mapozi ya kimahaba na wanawake wenzake, alishawahi pia kuonekana katika pozi tata na mwigizaji Aunt Ezekiel.

KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP

*********

JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:

KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA

INSTAGRAM: @Globalpublishers

TWITTER: @GlobalHabari

FACEBOOK: @GlobalPublishers

SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers

GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com

HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz

Leave a Comment