Na Nicodemus Jonas
ANACHOONGAA! Baada ya kuhakikishiwa kucheza mechi zote kuziba pengo la Ramadhan Kessy, beki wa kulia wa Simba, Mrundi, Emery Nimubona, amesema namba hiyo ilikuwa yake tangu zamani, lakini Kessy akapata bahati tu kuwa chaguo la kwanza.
Beki wa kulia wa Simba, Mrundi, Emery Nimubona.
Nimubona aliyesaini miaka miwili Msimbazi mwanzoni mwa msimu huu, amekuwa chaguo la pili mbele ya Kessy lakini sasa ana uhakika wa kucheza katika mechi tano za ligi kuu walizobakiza kufuatia Kessy kufungiwa mechi tano kwa kosa la kumchezea rafu mbaya fowadi wa Toto, Edward Christopher.
Akizungumza na Championi Jumatano, Nimubona alisema Kessy hakupewa kipaumbele kwa kumzidi kiwango, bali alipata bahati ya kupendwa na kocha.
“Sisemi kama ni mbaya, ila siamini kama Kessy kiwango chake kinazidiana na changu. Chochote anachokifanya nakifanya, sioni ni kitu gani naweza kujifunza kwake, maana tunalingana viwango, sema tu ni bahati tu ya kupangwa na kocha,” alisema beki huyo anayehimili pia kiungo wa kulia.
KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP
*********
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz

