×

Kisa talaka… Thea, mike wapelekana kanisani

NDOAYATHEA Mike Sangu na aliyekuwa mkewe, Salome Urassa ‘Thea’.

Na Hamida Hassan

Mastaa wa Filamu Bongo waliokuwa wanandoa, Mike Sangu na Salome Urassa ‘Thea’ wamepelekana kwa padri wa Kanisa  la Katoliki Parokia ya Mwananyamala jijini Dar kwa ajili ya hatua ya kutalikiana.

Chanzo kilicho karibu na mastaa hao kilidai kuwa, Thea ndiye aliyekusanya picha anazoposti Mike kupitia ukurasa wake wa Instagram akiwa na mpenzi wake wa sasa aitwaye Eliza na kuzipeleka kwa mchungaji ili kushawishi apewe talaka yake.

Ili kujua ukweli wa habari hiyo, mwandishi wetu alimtafuta Mike, alipopatikana alisema: “Ni kweli niliitwa nikajieleza ingawa habari hizi nisingependa ziandikwe magazetini kwa sababu bado ziko ngazi ya kanisani,” alisema Mike huku Thea akigoma kuongea chochote akidai ni mambo yake binafsi.

KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP

*********

JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU

KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA

INSTAGRAM: @Globalpublishers

ERIC SHIGONGO INSTAGRAM: @ericshigongo

TWITTER: @GlobalHabari

FACEBOOK: @GlobalPublishers

SUBSCRIBE YOU TUBE: Global TV Online

GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com

HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE:@shigongotz

Leave a Comment