×

Rais Magufuli, Dk Mpango waipangua safu ya Bodi ya Benki ya TIB

john-magufuliRais Dk. John Magufuli.

Dar es Salaam

Rais Dkt. John Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo  (TIB) Profesa William Lyakurwa.

Kufuatia hatua hiyo, kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 9 (2) cha ya Sheria ya mashirika ya umma,  Rais amemteua Profesa Palamagamba Kabudi kushika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB kwa kipindi cha miaka mitatu.

Kufuatia mabadiliko hayo, Waziri wa Fedha na Mipango Dk Philip Mpango  kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria ya sheria ya tafsiri za sheria   ametengua uteuzi wa Wajumbe TIB.

Dk  Mpango ameteua wajumbe wapya wa Bodi wafuatao kwa kipindi cha miaka mitatu, Brigedia Mabula Mashauri, Dk Razack Lokina, Rose Aiko, Profea Joseph Bwechweshaija, Said Seif Mzee, Dk Arnold  Kihaule, Maduka Kessy na Charles Singili. Uteuzi    unaanza leo.

1.jpeg

Leave a Comment