×

Usajili uliokamilika Ulaya

Ibramovic man u (5)LONDON, England

HIVI sasa kele za usajili zimepamba moto barani Ulaya. Mchuano ni mkali, kila kocha anataka kuimarisha kikosi chake. Championi Jumatatu kwa msaada mkubwa wa mtandao, linakuletea dili ambazo zilikamilika wiki iliyopita na nyingine zinakaribia kabisa kukamilika huku zikiwa zimebaki wiki sita tu kabla ya dirisha la usajili kufungwa mwishoni mwa Agosti:

GOMIS ANAKWENDA UFARANSA

Bafetimbi Gomis yupo njiani kuelekea Ufaransa. Straika huyo Mfaransa aliifungia Swansea mabao saba msimu uliopita lakini yupo huru kuondoka. Ameachwa kwenye kikosi kilichokwenda Marekani kujiandaa na msimu mpya na yupo karibu kutua Marseille kwa mkopo.

JORDON IBE ATUA BOURNEMOUTH

Winga huyo ameiacha Liverpool kwa dau la pauni milioni 15, Ijumaa iliyopita.

KANTE HUYOO CHELSEA

N’Golo Kante yupo karibu kabisa kutangazwa kama mchezaji mpya wa Chelsea akitokea Leicester. Kante amekubali kusaini mkataba wa miaka mitano kwa dau la pauni milioni 30.

MORENO ATUA KWA GUARDIOLA

Manchester City ambayo hivi sasa ipo chini ya kocha Pep Guardiola, imekamilisha usajili wa nyota kinda wa Colombia, Marlos Moreno. Fowadi huyo, 19, ametokea Klabu ya Atletico Nacional ya nchini kwao na inasemekana ni moto kwelikweli. Amenaswa kwa dau la pauni milioni 8.23.

MATIP RASMI LIVERPOOL

Beki kisiki Joel Matip amenaswa na mikono ya Jurgen Klopp katika kikosi cha Liverpool. Mcameroon huyo, 24, amejiunga na kikosi hicho kama mchezaji huru akitokea Schalke ambayo ameitumikia kwa miaka 16.

ROMA YAMNASA JESUS

AS Roma imethibitisha kumsajili beki Juan Jesus kutoka Inter Milan. Ametua kwa mkopo mrefu wa msimu wa dau la pauni mil 1.7.

KLUIVERT AULA PSG

Fowadi wa zamani wa Ajax, Barcelona na Newcastle, Patrick Kluivert raia wa Uholanzi, ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Soka wa Klabu ya PSG ya Ufaransa.

SUBOTIC ATUA MIDDLES-BROUGH

Middlesbrough wamemnasa beki wa kati Mserbia, Neven Subotic kutoka Borussia Dortmund. Amesaini mkataba wa miaka mitatu kwa dau linalosemekana kuwa ni pauni milioni nane.

NEGREDO ATUA MIDDLESBROUGH KWA MKOPO

Middlesbrough imekubaliana na Valencia kumchukua Alvaro Negredo kwa mkopo. Straika huyo wa zamani wa Man City, alitarajiwa kupata vipimo vya afya wikiendi iliyopita. Valencia imemuondoa baada ya kumpata Mreno, Luis Nani. Negredo aliwahi kuifungia City mabao 23 katika michezo 48 kwa msimu kabla ya kuondoka kikosini hapo.

GIACCHERINI ATUA NAPOLI

Kiungo mshambuliaji aliyeng’ara kwenye Euro 2016 akiwa na Italia, Emmanuele Giaccherini, 31, amekamilisha usajili wake katika kikosi cha Napoli akitokea Sunderland ambayo msimu uliopita ilimtoa kwa mkopo katika kikosi cha Bologna.

SKRTEL AJIUNGA FENERBAHCE

Usajili wa beki wa Liverpool, Martin Skrtel katika kikosi cha Fenerbahce umeshathibitishwa.

Raia huyo wa Slovakia alifanyiwa vipimo wiki iliyopita na kuhitimisha miaka yake nane katika kikosi cha Liver. Amenaswa kwa dau la pauni mil 5.5.

DIGNE ATUA BARCELONA

Liverpool ilitupa ndoano kwa beki wa kushoto Mfaransa, Lucas Digne, kabla ya kuitosa ofa hiyo na mahaba yake kuyaelekeza Barcelona ambayo imemnasa kwa dau la pauni mil 16.7. Msimu uliopita, alikuwa akiichezea Roma kwa mkopo akitokea PSG.

BENATIA ASAINI JUVENTUS

Juventus imekamilisha usajili wa beki Mmorocco, Medhi Benatia kutoka Bayern Munich. Nyota huyo, 29, alishindwa kupata nafasi ya kutosha Bayern ambayo aliichezea tangu 2014 tu. Kutua kwake kunaweza kumfanya Leonardo Bonucci aende Manchester City.

MAN CITY YAMNASA SANE

Manchester City imekamilisha usajili wa kiungo mpambanaji Leroy Sane kutoka katika kikosi cha Schalke. City imempa kiungo huyo mshambuliaji ofa ya mkataba wa miaka minne kwa dau la pauni milioni 42. City inamchukulia Sane kama kinda atakayekuja kuitikisa dunia hivi karibuni. Msimu uliopita alifunga mabao tisa na kutoa pasi za mabao saba.

WACHEZAJI WENGINE AMBAO WAMESHASAJILIWA (ENGLAND TU)

Arsenal:

Granit Xhaka – Gladbach, pauni 34m

Takuma Asano – Hiroshima, imefichwa

Burnley:

Jamie Thomas – Bolton, huru

Robbie Leitch – Motherwell, huru

Bournemouth:

Lys Mousset – Le Havre, pauni 5.4m

Emerson Hyndman – Fulham, pauni 0.75m

Nathan Ake – Chelsea, mkopo

Lewis Cook – Leeds, pauni 10m

Chelsea:

Michy Batshuayi – Marseille, pauni 33.2m

Crystal Palace:

Andros Townsend – Newcastle United, pauni 13m

Steve Mandanda – Marseille, huru

James Tomkins – West Ham, pauni 10m

Everton:

Maarten Stekelenburg – Fulham, imefichwa

Bassala Sambou – Coventry, kufidia

Chris Renshaw – Oldham, imefichwa

Hull:

Jonathan Edwards – Peterborough, huru

Will Mannion – Wimbledon, kufidia

Leicester:

Nampalys Mendy – Nice, pauni 13m

Ron-Robert Zieler – Hannover 96, pauni 2.6m

Luis Hernandez – Sporting Gijon, huru

Raul Uche Rubio – Rayo Vallecano, imefichwa

Ahmed Musa – CSKA Moscow, imefichwa

Liverpool:

Sadio Mane – Southampton, pauni 36m

Loris Karius – Mainz, pauni 4.7m

Joel Matip – Schalke, huru

Man City:

Ilkay Gundogan – Dortmund, pauni 21m

Nolito, Celta Vigo, pauni 13.8m

Oleksandr Zinchenko – FK Ufa, imefichwa

Aaron Mooy – Melbourne City, huru

Man United:

Zlatan Ibrahimovic

Eric Bailly – Villarreal, pauni 30m

Henrikh Mkhitaryan – Dortmund, pauni 26.3m

Middlesbrough:

Marten de Roon – Atalanta, pauni 12m

Viktor Fischer – Ajax, pauni 3.8m

Bernardo Espinosa – Sporting Gijon, huru

Jordan McGhee – Hearts, mkopo

Victor Valdes – huru

Southampton:

Nathan Redmond – Norwich, pauni 11m

Pierre-Emile Hojbjerg – Bayern Munich, imefichwa

Stoke City:

Hawajatangaza

Sunderland:

Hawajatangaza

Swansea:

Leroy Fer – QPR, pauni 4.75m

Mike van der Hoorn – Ajax, imefichwa

Tyler Reid – Manchester United, imefichwa

George Byers – Watford, huru

Tottenham:

Vincent Janssen – AZ Alkmaar, pauni 18.6m

Victor Wanyama – Southampton, pauni 11m

Watford:

Isaac Success – Granada, pauni 12.5m

Christian Kabasele – Genk, pauni 5.8m

Jerome Sinclair – Liverpool, huru

Juan Camilo Zuniga – Napoli, mkopo

West Brom:

Matt Phillips – QPR, pauni 5.5m

West Ham:

Manuel Lanzini – Al Jazira Club, pauni 9.4m

Toni Martinez – Valencia, pauni 2.25m

Havard Nordtveit – Gladbach, huru

Sofiane Feghouli – Valencia, huru

Gokhan Tore, Besiktas, mkopo

Domingos Quina – Chelsea, huru

Ashley Fletcher – Man United, huru.

Leave a Comment