Stori: Gladness Mallya
MWANADADA asiyeishiwa matukio Bongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’ amefunguka kuwa hajawahi kuachana na staa wa muziki Alikiba Saleh kama watu wanavyodhani, bali bado wapo wanaendelea na mapenzi.
Akipiga stori na Za Motomoto News, Gigy alisema japokuwa Alikiba yupo na Jokate Mwegelo, lakini bado ni mpenzi wake kwani walikotoka ni mbali hivyo haoni wivu wala tatizo kwenye suala hilo la ‘kushea’ mwanaume.
“Bado Alikiba ni mpenzi wangu, pale mmoja wetu anapomuhitaji mwenzake huwa tunatafutana, suala la Jokate kuwa na ujauzito wake wala haliniumizi,” alisema Gigy Money.

