×

Ajali ya Treni Yaua 4 na Kujeruhi 49

ttreni-1 Watu wanne wamefariki dunia na wengine 49 wamejeruhiwa baada ya treni kuacha njia na kugonga mnara karinu na eneo la  O Porrino, Kaskazini Magharibi mwa Hispania.

ttreni-2Takribani abiria 60 walikuwa ni raia wa Ureno na inasemekana miongoni mwa watu waliofariki dunia ni pamoja na dereva wa gari moshi hilo.

Behewa moja limeharibika kabisa huku mwngine mawili yakiwa yamebondeka vibaya.

_91079952_04e0b7d3-b21f-4045-b916-791212bfff28 Vikosi vya uokoaji viliwahi kufika eneo la tukio na kufanikiwa kuwaokoa baadhi ya abiria na watumishi wa treni hiyo waliokuwemo ndani wakati likipata ajali karibu na mpaka wa Ureno.

_91080463_spainoporrinjuredepa9sepMnamo Julai 31 mwaka 2013, ajali kama hiyo ilitokea baada ya treni kuanguka karibu na Mji wa Santiago de Compostela, na kuuwa watu 79 huku wengine 170 wakijeruhiwa

Leave a Comment