Mmoja ya waanzilishi wa Facebook, Dustin Moskovitz amechangia $ 20m kwa Democrats, kusaidia kumbwaga mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya Republican, Donald Trump.
Dustin Moskovitz, ni mjasiriamali Silicon Valley mwenye utajiri wa dola bilioni 10, leo Ijumaa ametangaza kuwa yeye na kundi lake wanamuunga mkono mgombea urais kupitia wa Chama cha democratic, Bi. Hillary Clinton, hivyo watafanya jitihada zote kumsapoti mama huyo ili aingie Ikulu.
Moskovitz amekuwa ni mtu wa tatu kutoa msaada mkubwa wa pesa kwa ajili ya kumsaidia Clinton kuingia madarakani.