×

NEMC Yatoa Tathmini ya Uhifadhi wa Mazingira

Ofisa Mkuu wa Mazingira NEMC, Arnold Kisiraga akizungumza na wanahabari (hawapo pichani).

BARAZA la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), limetoa tathmini yake  katika kusimamia shughuli za utunzaji wa mazingira nchini chini ya sheria ya Utunzaji na Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004.

Kushoto ni Ofisa Mazingira Mwandamizi wa NEMC, Fredrick Mulinda akiwa katika mkutano huo.
Wanahabari wakichukua tukio hilo.

Hayo yameelezwa leo na Ofisa Mkuu wa Mazingira (NEMC), Arnold Kisiraga alipokuwa akizungumza na wanahabari  jijini Dar es Salaam ambapo pia alisema kuwa NEMC inayo mamlaka ya kukuza, kuchochea, kusimamia na kuunganisha masuala yote yanayohusiana na mazingira.

…Kisiraga akijibu maswali ya wanahabari yaliyokuwa yameulizwa.

Alifafanua kuwa baraza linawajibika kuhakikisha kuwa mazingira yanatunzwa ili kuwa na matumizi endelevu ya rasilimali, ustawi na maisha bora ya wananchi na ukaguzi wa mazingira na kutoa maelekezo mbalimbali yanayolenga kuboresha hali ya mazingira au kutoa makatazo mbalimbali ya kisheria yenye kudhibiti uchafuzi na uharibifu wa mazingira kutoka katika baadhi ya viwanda visivyozingatia sheria ya mazingira.

NA DENIS MTIMA/GPL