
Suala la uadilifu nchini hasa kwa upande wa viongozi ambao wengi wao ni wasomi waliobobea, limekuwa ni gumu kwa muda mrefu na linaonekana kuendelea hivyo hadi sasa. Uadilifu ambao huenda sambamba na uaminifu, kwa muda mrefu na kwa watu wengi zaidi waliokuwa kwenye uongozi, nafasi yake imechukuliwa na ubinafsi.