×

Kardinali Pengo Aongoza Kuuaga Mwili wa Askofu Msemwa

Kardinali Pengo akiaga mwili wa marehemu.

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo ameongoza waumini na Maaskofu katika kuuaga mwili wa Marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na Masasi Castor Paul Msemwa katika Misa iliyofanyika katika Kanisa la Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) Kurasini Jijini Dar es Salaam.

Katibu wa Rais Ngusa Samike akiaga mwili wa Marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na Masasi Castor Paul Msemwa mara baada ya Misa iliyofanyika katika Kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Mapadri nao wakipita mbele kuaga mwili wa Marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na Masasi Castor Paul Msemwa mara baada ya Misa katika Kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam..
Jeneza lenye mwili wa marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na Masasi Castor Paul Msemwa likiwa limebebwa na Mapadri wakielekea ndani ya Kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Askofu Mkuu wa jimbo Kuu la Dodoma Beatus Kinyaiya akizungumza kabla ya kuaga mwili wa marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na Masasi Castor Paul Msemwa katika kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.

Usipitwe na Matukio, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers

Android Bofya ===> Google Play

iOS Bofya ===>Apple Store

Leave a Comment