×

WAFANYAKAZI OFISI YA WAZIRI MKUU KUTOA HUDUMA KWA UFANISI

Baadhi ya Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakipita katika viunga vya Jiji la Dodoma kuelekea katika Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Jamhuri kushiriki sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani, leo tarehe  Mei Mosi, 2018.
Baadhi ya Wafanyakazi  wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakishiriki maandamano ya kuelekea katika Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Jamhuri kushiriki sherehe za Mei Mosi.
Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakipita mbele ya mgeni rasm wakati wa sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani.
Baadhi ya Wafanyakazi  wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia sherehe za siku ya wafanyakazi Duniani katika Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Jamhuri  Jijini Dodoma.

 

KATIKA  kusherehekea siku ya Wafanyakazi Duniani, wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wameungana na wafanyakazi wote Duniani kwa kujumuika na wafanyakazi wengine wa hapa nchini Jijini  Dodoma na kuahidi  kuendelea kutoa huduma kwa ufanisi kwa Watanzania.

 

Wakiongea kwa nyakati tofauti wakati wa sherehe hizo wafanyakazi hao, wamesema kuwa ofisi ya Waziri Mkuu kama mratibu wa shughuli zote za serikali nchini na kama mratibu wa shughuli za kazi na ajira nchini wataendelea kutekeleza majikumu hayo kwa uadilifu na ufanisi ili huduma zinazotolewa na serikali ziwe zenye tija kwa Watanzania.

 

Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na kuratibu shughuli zote za serikali ndani na nje ya Bunge pia inaratibu masuala mtambuka, kama  shughuli za maafa, Udhibiti wa matumizi ya madawa ya kulevya, vita dhidi ya UKIMWI, huduma kwa watu wenye ulemavu.

 

Aidha inahusika na  kuchapa nyaraka za uendesheshaji shughuli za serikali, masuala ya vyama vya siasa, masuala ya uchaguzi, masuala ya kazi, ajira na maendeleo ya vijana, pamoja na masuala ya uwekezaji na uwezeshaji wananchi kiuchumi.

 

Maadhimisho ya sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani mwaka huu zimebebwa na kauli mbiu ya “Uunganishaji wa Mifuko ya Jamii ulenge kuboresha mafao ya mfanyakazi”