×

Mafuriko Tanga: Noah Yatumbukia Mtoni, Wanane Wafariki – Video

WATU nane wamefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumamosi, Oktoba 26, 2019 baada ya gari aina ya Noah walilokuwa wakisafiria kutumbukia kwenye daraja katika eneo la Sindeni barabara kuu ya Handeni Korogwe, kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa ajali hiyo imetokea wakati wakitoka Handeni kwenda Tanga Mjini.