
SERIKALI ya Zambia imepitisha sheria inayohalalisha kilimo cha zao la bangi kwa sababu za kiuchumi na tiba.
Kwa hatua hiyo, taifa hilo linakuwa la hivi karibuni kabisa katika kuridhia matumizi ya bangi. Kwa mujibu wa taarifa ya Msemaji Mkuu wa Serikali ya Zambia, Dora Siliya, idhini ya kufanya biashara ya bangi ilitolewa na kikao maalumu cha baraza la mawaziri kilichoketi Desemba 4 mwaka huu.
Hata hivyo, bado haijaweza kuwa wazi kama matumizi ya bangi kwa sababu za kitabibu nchini humo pia yamehalalishwa.
Taifa hilo lililo kusini mwa Afrika, linajiunga na mataifa mengine ambayo yamehalalisha bangi au kuzingatia matumizi wa mmea huo kwa tiba, ikiwa na kusudio la kujinufaisha kibiashara.