×

Papa Francis Afanya Maamuzi Magumu Kuhusu Unyanyasaji wa Kingono

Papa Francis ametangaza mabadiliko makubwa kwa jinsi Kanisa Katoliki linavyoshughulikia kesi za unyanyasaji wa kingono kwa watoto na kukomesha kanuni ya “usiri” ambayo iliwaficha makasisi waliokuwa wakitenda vitendo hivyo hapo awali.

 

Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki Duniani ameondoa ‘usiri wa Kipapa’ katika kesi za manyanyaso ya kingono dhidi ya watoto wadogo zilizotendwa na makasisi. Pia, amefanya uhalifu wa umiliki na usambazaji wa picha chafu zinazohusisha watoto chini ya umri wa miaka 18 kuwekwa katika kundi la delicta graviora, yaani makosa mabaya zaidi.

 

Kwa maana hii, amefanya kuwa na uwezekano wa upatikanaji wa ushuhuda wa kesi kwa wachunguzi wa kiserikali.

 

Pia ameondoa siri zinazohusiana na utoaji taarifa, mashitaka na michakato ya maamuzi kuhusu kesi za dhuluma na vitendo vya kingono vilivyofanywa chini ya vitisho au matumizi mabaya ya mamlaka; kesi za unyanyasaji wa kingono wa watoto au watu walio katika mazingira magumu; kesi za ponografia ya watoto; kesi kuhusu kukosekana kwa kuripoti na kuficha wanyanyasaji kwa upande wa maaskofu na wakurugenzi wakuu wa taasisi za kidini.

Leave a Comment