×

DC Chongolo Awaahidi Neema Wakazi wa Nakasangwe

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo, akizungumza na wakazi wa Nakasangwe jana.

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo, jana (Jumanne) aliwaahidi wakazi wa Nakasangwe Kata ya Wazo Hill, Dar es Salaam, kumaliza mgogoro wa ardhi uliokuwa ukiwakabili kwa kuwapatia hati halali za kumiliki ardhi hiyo.

Baadhi ya wakazi waliohudhuria mkutano ambapo waliahidiwa kupewa hati za kumiliki makazi yao.

Hatua hiyo itamaliza mgogoro huo uliochukua muda mrefu, jambo ambalo liliwafanya wakazi hao kushangilia uamuzi huo.

 

Sehemu ya wakazi wakifuatilia kwa makini majadiliano katika mkutano huo.

Matatizo mengine aliyoahidi mkuu huyo wa wilaya kuyamaliza  ni pamoja na tatizo la maji ambapo alifika eneo hilo na maofisa wa mamlaka ya maji jijini Dar es Salaam (Dawasa) na shirika la umeme nchini (Tanesco)  ambao walieleza mipango ya kusambaza huduma hizo kwa wakazi hao ndani ya siku chache.

Mkutano ukiendelea. 

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL

Leave a Comment