
INASIKITISHA sana! Mwanamke mmoja amemwokoa mtoto wake kwa kumrusha kupitia kibarazani wakati ajali kubwa ya moto uliotokea na kuteketeza nyumba yao ya gorofa ya tatu huko Phoenix, Arizona, Marekani.
Inaripotiwa ndani ya nyumba alikuwepo mama na mtoto ambapo kwenye hiyo video mama anaonekana akimuokoa mtoto wake kwa kumrusha chini kupitia kibarazani na kutajwa kuwa mwanamke shujaa.
Kwa mujibu wa ABC NEWS, mama huyo alifariki kwa kuwa alikuwa ameungua sana lakini alipambana na kuhakikisha amefika kibarazani na kumrusha mtoto wake chini ambapo alidakwa na watu wawili.