×

Rais Magufuli: Kwani Hatuogopi Kufa? – Video

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli leo Jumatatu, Julai 20, 2020 amewaapisha viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni wakiwemo wakuu wa Mikoa wakuu wa Wilaya, wakurugenzi pamoja na Makatibu Tawala.

 

Miongoni mwa mambo aliyoyazungumzia Rais Magufuli ni haya;

“Nilikuwa napata taarifa leo kwamba wagombea wa ubunge na uwakilishi waliochukua fomu kupitia CCM ni 10,367, waliojaza na kurudisha ni 10,321 na ambao hawakurudisha ni hawakurudisha 46, katika nchi nzima. 

 

“Ninatumaini viongozi watasiamamia kura za maoni kwa haki bila mizengwe, ninatamani kura zikafanyike kama tulivyofanya kwenye Halmashauri Kuu, zihesabiwe hadharani anayepata zero apate hapo hapo anayepata zote hapo hapo, huu uwazi utaendelea kujenga umoja wa CCM.

 

Kwa walioapishwa;

“Nitashangaa sana miradi ya maji iache kutekelezwa hapa, iache kukalimika, iwe na wizi wakati walioko mbele ni mwanaume na mwanamama na wote ni Wahandisi. Nitasikitika kwanini niliwaonea wale wawili nikakuchagua wewe.

 

“Dkt. Seif ni Dokta ‘By Profession’. Amesoma akamaliza akapata PhD Uholanzi akaenda kwenye kituo cha Utafiti Ifakara. Miaka ya nyuma aliomba Ubunge Korongwe, hakuwa na hela wala nini alitaka kuwatumikia wanaKorogwe, akapigwa chini.

 

“Huyu Dkt. Kijazi, sikumteua kwa sababu kaka yake ni Katibu Mkuu Kiongozi, na hili nataka niliweke wazi undugu ni pembeni, amefanya kazi TANAPA vizuri tu na ndiyo maana nikasema imepatikana fursa akawe Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii..

 

“Katika baadhi ya Wakurugenzi waliokuwa wanafanya kazi vizuri katika Wizara ya maji walikuwa watatu, mmoja ni mwanamama. Wale wanaume ikabidi niwapige chini, nikamchagua mwanamama ili kusudi akashiriki kikamilifu katika kuwatua ndoo wanamama.
“Aswege amekuwa Afisa Utumishi Mbalali na mara nyingi amekuwa akikaimu Ukurugenzi na amekuwa akiletewa mizengwe na TAKUKURU. Ile mizengwe ikaisha na TAKUKURU wakamsafisha. Sasa mimi nikaona kama TAKUKURU wamesafisha kwanini mimi nimsafishe kwa kumteua?
Ndugu Chogelo katika maeneo yote aliyopangwa amefanya kazi vizuri. Tukaona anafaa kwenda Ilala. Unapopeleka DC kwenye Makao Makuu ya Nchi au sehemu kama Dar lazima aende yule aliyefanya kazi sehemu nyingine. Anafanya kazi vizuri sana.
“Tatizo hili nililipata pia kwa Wateuzi wawili wako hapa, Ndugu Aswege anatoka Mbalali na mwingine anatoka Moshi. Wote wanatoka Ileje, na inawezekana wanatoka Tarafa moja. Ilikuwa ngumu, unajikuta wote wanaofanya vizuri wapo sehemu moja.
Huyu aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Lindi. Enhe! CCM lazima iwemo ndio inatekeleza ilani ya Uchaguzi. Huyu ni mwalimu, amekuwa mwalimu wa shule ya msingi Nanyumbu. Alifanya kazi kaenda kusoma, akapata ‘degree’ ya kwanza na ya pili.
“Tuko salama, hata hapa ungekuta tumevaa #Barakoa. Kwani sisi hatuogopi kufa? Lakini #Corona iko mbali kule, ilimalizwa kabisa. Tulimuomba Mungu, tukamtanguliza Mungu na Mungu akatusikia. Kila mtalii anakayekuja atakuja na kuangalia Wanyama na kuondoka salama.
“Nakushukuru Jaji Mihayo na Wizara ya Maliasili, nimeanza kuona Watalii wanakuja wengi na ndege zinaleta Watalii wengi. Watu wameanza kuangalia na kuuona ukweli kuwa hapa Tanzania tuko salama. Endeleeni kulitangaza hili. Maadui zetu watazungumza mengi.
“Nawashukuru wote mliohudhuria. Katika mwezi huu tumekuwa tukikutana sana hapa katika kuapisha. Inawezekana tusikutane tena hapa. Matumaini yangu tumemaliza labda baada ya kampeni na kadhalika. Ninyi nafasi mmezijaza na sidhani kama mmoja wetu ataenda kutia nia,” mesema Magufuli.

⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:
⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8
⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx

⚫️ VISIT AMAZON: https://www.amazon.com/shop/globaltvo…

Leave a Comment