×

Lusajo, Bigirimana Wampa Hofu Sven

KOCHA Mkuu wa Klabu ya Simba, Sven Vandenbroeck, amekiri kuwa ubora wa safu ya ushambuliaji ya Namungo inayoongozwa na Reliants Lusajo na Blaise Bigirimana ni miongoni mwa vitu vinavyompa hofu kuelekea mchezo wao wa fainali ya Kombe la Shirikisho inayotarajiwa kupigwa wikiendi hii kwenye Uwanja wa, Nelson Mandela, Sumbawanga mkoani Rukwa.

 

Lusajo na Bigirimana msimu huu wameifungia Namungo mabao 22, hivyo kuifanya timu hiyo kuwa miongoni mwa timu zenye safu bora ya ushambuliaji ndani ya Ligi Kuu Bara.

 

Akiuzungumzia mchezo huo, Sven alisema: “Licha ya kwamba timu yetu inapewa nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi kwenye fainali ya FA dhidi ya Namungo kutokana na ubora tulionao lakini kwa upande wangu natarajia kuwa mchezo huu utakuwa mgumu hasa kutokana na ukweli kwamba Namungo ni timu iliyojengwa vizuri.

 

“Wana safu ya kiungo iliyo bora na kuna wale washambuliaji wao wawili, Reliants Lusajo na Bigirimana Blaise ambao ni hatari sana hivyo hatupaswi kuwapa nafasi hata kidogo.”

 

AFUNGAJI BORA

Kagere – Simba Sc 22

Mhilu – Kagera Sugar 13

Wazir Jr – Mbao Fc 13

Mapunda – Mbeya City 12

Lusajo – Namungo Fc 12

Chirwa – Azam Fc 12

Nonga – Lipuli Fc 11

Saliboko – Lipuli Fc 11

Blaise – Namungo Fc 11

Molinga – Yanga Sc 11.

JOEL THOMAS | Dar es Salaam

Leave a Comment