
BAADHI ya wananchi wa Rwanda wamejikuta katika wakati mgumu baada ya kupewa adhabu ya kukaa saa kadhaa na kusikiliza hotuba, na matangazo mbalimbali kuhusu ugonjwa wa Covid-19 katika uwanja wa michezo wa Nyamirambo, mjini Kigali nchini humo — wakati wa usiku.
Adhabu hiyo imetolewa kwa wananchi hao baada ya kukiuka sheria ya kupambana na Covid-19, walipokutwa wakitembea mitaani bila kuvaa barakoa, kama ambavyo sheria ya nchi hiyo inavyotaka ikiwa ni moja ya njia za kupambana na ugonjwa huo wa mlipuko.