
LINDI: Agosti17, 2020: Wadau mbalimbali wa kilimo cha zao la korosho nchini wameonesha kuvutiwa na huduma mpya ya NBC Shambani hukuwakibainisha ujio wa huduma hiyo maalumu kwa ajili ya wakulima utaondoachangamoto za muda mrefu ikiwemokutopata mikopo kwa wakati sahihi.
Wakizungumzawakati walipotembelea banda la huduma za benki hiyo kwenye mkutano mkuu wawadau wa korosho uliofanyika mwishoni mwa wiki mkoani Lindi, baadhi ya wadau wazao hilo wakiwemo wakulima, wafanyabiashara wa pembejeo za kilimo nawasafarishaji wa zao hilo walisema miongoni mwa changamoto zinazowakabili kwasasa ni kutopata mikopo kwa wakati sahihi hivyo wanaamini ujio wa huduma hiyompya utaondoa changamoto hiyo.
“Lichaya uwepo wa huduma nyingi za kibenki kwa ajili ya wakulima bado tumeendeleakukabiliwa na changamoto kadhaa za huduma za kifedha ikiwemo ucheleweshwaji wamikopo na tunapoipata inakuwa sio wakati sahihi na hivyo kusababisha wengi wetukuitumia kwa matumizi yasiyokusudiwa. Ni matarajio yetu ujio wa huduma NBCShambani utatatua changamoto hii na sisi tupo tayari kuiopokea,’’ alisema BwSalum Muhila, mkulima wa korosho kutoka wilaya ya Liwale, mkoani Lindi.

Awali,akifafanua kuhusu huduma hiyo kwa wadau hao, Mkuu wa Kitengo cha wateja Wadogona wa Kati kutoka Benki ya NBC Bw Raymond Urassa alisema inalenga wadau wotewanaojihusisha na mnyororo wa biashara ya Kilimo wakiwemo wasambazaji wapembejeo za kilimo, wakulima na wasafirishaji wa mazao ya kilimo na tayariimepoanza kutumiwa kwa wingi na wakulima wa zao la ufuta.
Alibainishahuduma hiyo inatoa fursa kwa wadau hao kuwa na akaunti ya vikundi vya wakulima kama vile AMCOS navikundi vingine pamoja na akaunti ya mkulima mmoja mmoja.
“Akaunti ya NBC Shambani kwa vikundi vya wakulima inawawezesha kuweka fedha bilaada ya uendeshaji wa akaunti huku piavikundi vikifaidika kwa faida nyingiikiwemo kutokatwa gharama za uendeshaji wa akaunti kila mwezi, kupata taarifaza akaunti bure sambamba na kutokatwa makato ya kuhamisha fedha wakati wakulipa wakulima wenye akaunti NBC,’’alifafanua.
Akizungumzakwenye mkutano huo, Waziri wa Kilimo Bw Japhet Hasunga alibainisha kuwa katikakubabiliana na changamoto kadhaa zinazowakabili wakulima ikiwemo kutotambulikarasmi kwenye taasisi za kifedha tayari serikali imeanza kutoa vitambulishomaalum kwa ajili yao vitakavyowatambulisha hususani wanapohitaji huduma zakifedha.
“Vitambulishohivyo vya kisasa vitakuwa na ‘chip’ maalumu itakayobeba taarifa zote muhimukuhusu mkulima hatua ambayo tunaamini itazirahisishia taasisi za fedha mlolongomrefu wa kukusanya taarifa za wadau hao na hivyo kuwapatia mikopo kwa wakati,’’alisema Waziri Hasunga ambae katika mkutano huo alikabidhi vitambulisho hivyovya mfano kwa wakulima 15 wa awali.
“Zaidipia kwasasa serikali tunatathimini upya sera ya masoko ikiwemo suala zima lakilimo cha mkataba ili wakulima wetu waweze kujua bei za bidhaa zao mapemakabisa,’’ alibainisha.
