×

Twanga Ilivyokinukisha Usiku Wa Kuamkia Leo

Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ usiku wa kuamkia leo Jumamosi ilipiga bonge la shoo kwenye Ukumbi wa Baa ya T Garden iliyopo Sinza Jijini Dar ambapo nyomi la mashabiki lilihudhuria.

Bendi hiyo inayotamba na ngoma yake mpya ya Mapenzi Sigala Kali utunzi wake, Chaz Baba ‘Kingunge’ mashabiki wamekuwa wakidata sana na kibwagizo cha ngoma hiyo kisemacho msaliti “Msaliti hata weeewe eewe” na uchezaji wa staili ya Maria Roza “Mariaaa eeeh Maria Roooza”

Angalia matukio yalivyokuwa.

Mkurugenzi wa Twanga Luiza Mbutu akimuangalia kijana wake, Chaz Baba anavyoimba wimbo wake wa Mapenzi Sigala Kali.
Kiongozi wa wanenguaji wa Twanga, Super Nyamwela (katikati) akionesha mavitu na wanenguaji wake, Stellah Kiuno (kushoto) na Maria Soloma.
Shabiki akisugua kisigino ilipofika muda wa swaga hiyo huku akichombezwa na Luiza Mbutu mbele yake.
Miraji Shakashia ‘Shakazulu’ akiwajibika na gitaa lake kuhakikisha anawanogesha mashabiki.
Kalala Junior kama kawaida yake akiimba kwa swaga ya kulalamika huku akipigwa jicho na Luiza.

Mcharaza besi gitaa, Jojoo Jumanne na muimbaji, Saleh Kupaza wakiwa kazini.                                           

HABARI/PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL

Leave a Comment