
Benki ya Akiba Commercial imezindua wiki ya huduma kwa wateja katika hafla iliyofanyika tawi lao la Tegeta jijini Dar kwa kuungana na wateja wao katika maadhimisho hayo.
Katika uzinduzi huo maofisa wa benki hiyo walizungumza na wateja wao kwenye tawi hilo na wengine kuwatembelea kwenye biashara zao.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano Benki ya Akiba Commercial, Dora Saria amesema dhumuni kubwa la hafla hiyo ni kuwashukuru wateja pamoja na watoa huduma wao.
Baada ya uzinduzi huo maofisa wa benki hiyo walikata keki pamoja wateja wao na kisha kupata brekfast ya pamoja katika kuonesha mshikamano na upendo walionao kwao.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Dora alisema;
“Katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja tumeamua kuwapa zawadi mbalimbali wateja wetu walioshinda katika zoezi la kuweka akiba kubwa zaidi.
“Pia katika wiki hii ya Huduma kwa Wateja tumezindua tena kampeni ya kujiwekea akiba hivyo tunawashauri wananchi wote kufungua akaunti Benki ya Akiba na kushiriki katika zoezi hilo ili nao waweze kufaidikia na huduma hiyo.

“Pamoja na kuwapa zawadi wateja wetu pia tumetambua na mchango wa staff wetu ambapo tumeangalia idara mbalimbali na kuteua wafanyakazi bora katika kila idara na kuwatunukia vyeti ili nao waone jinsi taasisi wanayofanyia kazi jinsi inavyowathamini”. Alisema Dora.
Katika kumalizia Dora amesema benki yao imeanzisha huduma ya malipo ya serikali ambayo inaitwa Akiba Mobile.

Kupitia huduma hiyo mteja wa benki hiyo ataweza kufanya malipo mbalimbali ya serikali kama vile faini za trafiki, kulipia leseni, kodi za majengo na malipo mengine ya serikali. Alimaliza kusema. HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL