
Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom imeamua kufanya jambo kwa kuwafungulia duka wateja wa kampuni hiyo katika eneo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Akizungumza kwenye uzinduzi wa duka hilo, Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wa Vodacom, Harriet Lwakatare amesema wameamua kufungua duka hilo kwa ajili ya kuwasaidia wateja wao wa maeneo hayo.

“Hili eneo lina pilikapilika nyingi ikiwemo abiria wanaoingia na kutoka hapa nchini ambapo wanahitaji huduma ya uhakika wa mawasiliano.
“Hivyo basi tumeona ni viuzuri tukiwawekea duka letu hapa ili waweze kutatua changamoto ya kimawasiliano”. Alisema Harriet.

Baada ya kusema hayo, Harriet aliwaongoza watoa huduma wa kampuni hiyo kukata keki na kufungua shampeni wakisherehekea uzinduzi wa duka hilo pamoja na kusherehekea wiki ya Huduma kwa Wateja.

Katika hafla hiyo, Harriet aliwapa zawadi watoa huduma bora kwa kampuni hiyo na kuwahamasisha wengine kujituma zaidi ili nao taasisi wanayofanyia kazi iwazawadie kama wenzao hao.