
Mkuu wa Udhibiti Hatari na Utekelezaji wa Benki ya NMB, Victor Rugeiyamu, kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Mkalapa, wilayani Masasi – mkoani Mtwara. Kushoto ni Meneja wa NMB Kanda ya Kusini, Janeth Shango.
Benki ya NMB imetoa msaada wa vifaa vya hospitali; vitanda, magodoro na mashuka vyenye thamani ya shilingi milioni kumi na tano kwa hospitali za halmashauri za wilaya za Tarime vijijini (Mara), Ushetu katika wilaya ya Kahama (Shinyanga) na Mikumi – wilaya ya Kilomero (Morogoro).
Vifaa hivyo vimekabidhiwa wakati Benki hiyo ikizindua huduma mpya tatu za kibabe katika maeneo mbali mbali nchini; Namba ya WhatsApp 0747333444, njia ya digitali ya kutoa maoni kwa mfumo wa kuscan QR pamoja na mfumo wa kurudisha token za umeme (token retrieval) wakati wakiadhimisha wiki ya huduma kwa wateja.

mashuka kutoka kwa Afisa Mkuu Rasilimali Watu wa NMB, Emmanuel Akonaay kwa ajili ya hospitali ya Wilaya
ya Ushetu – Kahama.
Hospitali mpya ya Halmashauri ya wilaya ya Tarime iliyopo Nyamwanga ilikabidhiwa vitanda saba vikiwemo viwili vya kujifungulia na magodoro. Akipokea msaada huo Katibu Tawala wa wilaya ya Tarime, John Marwa alisema msaada huo utaboresha huduma za matibabu katika hospitali hiyo ambayo inahudumia zaidi ya watu 300,000 wakiwemo wamama wajawazito.

Katika hatua nyingine, Benki hiyo pia imetoa msaada wa meza na viti 50 kwa ajili ya shule ya Sekondari ya Mkalapa iliyopo Ndanda wilaya ya Masasi, ili kupunguza uhaba wa madawati shuleni hapo.

Benki ya NMB kupitia kitengo chake cha Uwajibikaji kwa Jamii, imekua na utaratibu wa kurejesha
sehemu ya faida yake ya asilimia moja kwa jamii kusaidia katika sekta ya afya, elimu na majanga.