ALIYEKUWA mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema, ameachiliwa na polisi nchini Kenya baada ya kukamatwa kwa madai ya kuingia nchini humo kinyume na sheria.
Kwa mujibu wa wakili wake, George Wajackoyah, Lema ambaye alikua ameambatana na familia yake alikuwa akielekea jijini Nairobi kwa ajili ya kutafuta makazi ya muda baada ya kudai kutishiwa maisha.
Sasa mamlaka za Kenya zimemruhusu Lema na familia yake kubaki nchini humo wakati akiendelea na taratibu za kuwa mhamiaji wa muda.
