SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, amesitisha shughuli za Bunge kwa muda wa nusu saa ili kujiandaa kupokea bahasha yenye jina la uteuzi wa Waziri Mkuu kutoka kwa Rais John Magufuli.
Jina la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajiwa kufikishwa leo bungeni ambapo wabunge watalipigia kura za ndiyo au hapana.
