×

Magazeti ya Championi, SportXtra Yagawa Tiketi Mechi ya Simba vs Platnum

Mkuu wa Idara ya Masoko ya Global Publishers, Adam Anthon (kushoto) akimkabidhi tiketi msomaji wa magaezeti ya Championi na Spoti Xtra.
Ofisa Masoko wa Global Publishers, Samwel Shigongo (kushoto) akimpatia msomaji tiketi kwa ajili ya kuingilia uwanjani.
Maofisa masoko wa Global wakiwaelekeza jambo baadhi ya wasomaji wa magazeti ya Championi na SpotiXtra.
Mkuu wa kitengo cha Masoko Cha Global Publishers,Adam Anthon (kushoto) akimrudishia fedha msomaji wa magaezeti ya Championi na Spoti Xtra baada ya kukutwa akilisoma gazeti hilo.
Mkuu wa kitengo cha Masoko Cha Global Publishers,Adam Anthon (kulia) akimkabidhi tiketi msomaji wa magaezeti ya Championi na Spoti Xtra.

 

Timu ya Masoko kutoka Kampuni ya Global Group kupitia magazeti ya Championi na spotiXtra imeingia mtaani na maeneo ya Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es salaam kwenye michuano ya ligi ya mabingwa Afrika, Simba SC na FC Platinum ya Zimbabwe ambapo mchezo huo niwa pili wa Raundi ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Hii imekuwa kawaida ya Kampuni ya Global Publishers kurudisha fadhila kwa wasomaji wake ikiwa ni pamoja na kuwapa zawadi mbalimbali.

“Hii imekuwa desturi kurudisha fadhila kwa wasomaji wetu kwani wamekuwa wakituunga mkono sana, hivyo ni jambo jema kuwarudishie kile tunachokipata kutoka kwao, ili na wao wajisikie kama familia ya Championi na Spoti Xtra,” alisema Anthony Adam ambaye ni Mkuu wa Idara ya Usambazaji wa Global Publishers wakati wakigawa tiketi hizo kwa mashabiki.

 

Leave a Comment