×

Rais wa Msumbiji Kufanya Ziara Nchini

Rais Felipe Nyusi wa Msumbiji anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku mbili nchini kuanzia kesho Januari 11.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Geita, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi amesema kuwa, Rais Nyusi alipanga kufanya ziara nchini tangu mwaka 2020, lakini kutokana na ratiba ya Uchaguzi Mkuu hapa nchini, alisogeza mbele ziara hiyo.

Leave a Comment