
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva Zuchu amesema kuwa hakutegemea mapokezi aliyoyapata kutoka kwa Watanzanai kwani lengo lake lilikuwa labda miaka miwili ndio afikie mafanikio haya.
“Sijasababisha sukari ipande bei kama inavyoelezwa msinigombanishe na Serikali,” amesema Zuchu.
Mbali na hilo Mbosso amemshauri Zuchu na kumweleza kuwa mashabiki wa muziki Tanzania hawakupata msanii sahihi wa kike wa kumpenda kwa miaka mingi sana na kwa sasa wamempa Zuchu ndio maana wanaupenda mkubwa sana kwake.