×

Mafuriko Jangwani Mwisho 2022

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Ummy Mwalimu amemuagiza Msimami wa Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es salaam (DMDP) Eng. Humphrey Kanyenye kuhakikisha wanakamilisha kazi ya uboreshaji wa eneo la Jangwani Jijini Dar es salaam ili kuzuia mafuriko yanayoathiri eneo hilo kila mwaka.

‘Nataka mwaka 2022 tusahau kabisa kuona mafuriko pale Jangwani kazi za uboreshaji wa eneo hilo zifanyike kwa haraka na kwa ubora unaotakiwa wakandarasi angalieni hili na mlifanyie kazi’ Mhe Ummy Mwalimu

Ziara Mkoani Dar es Salaam
Ukaguzi wa Mradi wa DMDP
Juni 5, 2021.

Leave a Comment