Mwenyekiti wa C&S Forum, Dkt. Emmanuel Chao akifungua mafunzo hayo.
Asasi ya C&S imeendesha jukwaa la kuhamasisha vijana wadogo kushika nyadhifa za ukurugenzi na ngazi zingine za juu kwenye taasisi mbalimbali ikiwemo serikalini.

Jukwaa hilo liliyoongozwa na Mwenyekiti wa C&S Forum, Dkt. Emmanuel Chao imefanyika kwenye Hoteli ya Slip Way iliyopo Msasani, Dar na kuhudhuriwa na vijana mbalimbali wakiwemo vijana wadoha go waliofanikiwa kushika nyadhifa za juu kiutendaji.

Miongoni mwa vijana waliojitokeza kwenye warsha hiyo ni kijana wa mfano Foseph Fungo ambaye Meneja wa Mkoa wa NSSF wa Kinondoni.

Vijana Warsha hiyo pamoja na kuongozwa na Dkt. Chao pia iliendeshijana wadogo waliofanikiwa kushika nyadhifa za juu kwenye taasisi wanazofanyika kazi akiwemo Mkurugenzi wa Jackson Group, Kelvin Twissa, Reuben Ndege ambaye ni Brand Strategic wa Clouds Media, Diana Laizer ambaye ni Mkurugenzi wa African Consumer Chice Awards na wengineo.

Akizungumza baada ya uzinduzi wa jukwaa hilo pamoja na uzinduzi wa kitabu cha CEO, Dkt. Chao alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwapata viongozi wa nyadhifa za juu wa kizazi kipya ili kufikia haraka maendeleo yanayokwenda na wakati.

HABARI/PICHA:RICHARD BUKOS / GPL