
LEO AGOSTI 10, 2021 ni siku muhimu kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Group LTD na Mbunge wa Buchosa, Eric James Shigongo, ambaye anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.
Wafanyakazi wote wa Kampuni ya Global Group iliyopo Sinza Mori jijini Dar, tunakutakia heri ya kuzaliwa.
Tunatambua mchango wako ni mkubwa kwa wafanyakazi wote wa Global Group na Tanzania kwa jumla, hivyo tunakuombea miaka mingi zaidi, Mwenyezi Mungu akulinde, akuongoze na akupe nguvu zaidi ya kulifikisha taifa hili mbali.
Heri ya Kuzaliwa Eric James Shigongo!